Katika vurugu hizo, askari mmoja amejeruhiwa katika paji na uso huku gari la Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero Wallace Karia aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajili SM 4503 likivunjwa vioo.
Pia waandishi wa habari wa TBC, ITV na Global Publishers waliofika eneo la tukio walipigwa mawe na wakulima.
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Anthony Mtaka alipohojiwa na waandishi nje ya kituo cha Polisi Dakawa alilaani kitendo kilichofanywa na wakulima hao na kulipongeza jeshi la polisi kwa kutumia busara wakati wa vurugu hizo licha ya kupigwa mawe.
Hadi mwandishi wa mtandao huu anaondoka eneo hilo bado barabara ilikuwa imefungwa.
-Gpl
