Pata Habari Motomoto kwa kuandika E-mail yako hapo chini.


HUU NDIO MSIKITI ANAO UJENGA MZEE MAJUTO NYUMBANI KWAKE....ANGALIA PICHA HAPA

Ni kitu kizuri kuona binadamu yeyote anapojisogeza karibu zaidi na Mungu, mwigizaji/mchekeshaji staa wa Tanzania ambae kwa sas


Katika kijiji kipya atakachohamia siku kadhaa zijazo huko Tanga, Mzee huyu ameamua kujenga msikiti mdogo mpya wa matofali ya cement ambao atautumia kuswali pamoja na watu wengine ambapo mwanzoni alikua amejenga huo wa udongo hapo juu lakini akabadili mawazo hata kabla ya kuanza kuutumia, sasa anajenga wa kisasa zaidi.
 

TAZAMA PICHA ZA JUKWAA LA FIESTA DAR LINAVYOTENGENEZW


10Hapa bado haijakamilika, ni stage ambayo kukamilika kwake inachukua siku kumi ikiwa inatengenezwa… ni stage ambayo itakua na winch ya kupandisha wasanii kuja kufanya show, kutakua na screen za kisasa zaidi kuonyesha kila kinachoonekana kwenye stage.. 7Kama unavyoona kwa mbali, kwa mara ya kwanza Fiesta hii backstage yake imejengewa nyumba ya kisasa zaidi na ndefu kwenda juu, ndani yake kutakua na baa, screen kubwa, makochi ya  kisasa kwa ajili ya watakaokuwepo hapo. 6 8 9Hii ni stage nyingine 3 4 1Ukiangalia kwa makini hapa kuna stage mbili kubwa ambazo zimeunganishwa na barabara ambayo inamuwezesha msanii kutembea juu huku mashabiki wakiwa pembeni kulia na kushoto yani… 2Hivyo ni baadhi tu ya vitu nimeamua kukupa kwa sasa mtu wangu,

MWANAUME AAMUA KUMYWESHA MPENZI WAKE TINDI KALI, KISA WIVU WA MAPENZI..

Jitendra Sakhpal akisindikizwa na polisi kuingia mahakamani. Msichana mdogo ameungua vibaya baada ya rafiki yake wa kiume aliyevunja naye uchumba kudaiwa kumtega walipokutana, kumlazimisha kunya tindikali na kumsukumia kwenye bahari.

Ripoti nchini India zinadai msichana huyo hapo kabla alikuwa mpenzi wa Jitendra Sakhpal, miaka 21, ambaye alikuwa amemchumbia, lakini alikataa kuolewa naye na kusitisha mahusiano hayo sababu familia yake haikumridhia mwanaume huyo asiye na ajira.
Baba wa msichana huyo aliripotiwa kuieleza polisi kwamba mvulana huyo alikuwa akiwasumbua, na ndugu mmoja wa kike alidai kwamba Sakhpal alitishia kumuua baba wa msichana huyo, kwa mujibu wa ripoti hizo.
Msichana huyo, ambaye hakutajwa jina, anaripotiwa kuwa mahututi kwenye Hospitali ya Thunga, mjini Mumbai.
Sakhpal amekamatwa na kushitakiwa kwa jaribio la mauaji.
Shambulio hilo limetokea Jumamosi huko Gorai Beach katika kitongoji cha magharibi mwa Mumbai. Wote ni wakazi wa Dahisar mjini Mumbai.
Msichana huyo mwenye miaka 18, mwanafunzi wa HSC ambaye ametokea Borivali, alikutana na Sakhpal wakati akiondoka chuoni Jumamosi, kwa mujibu wa Polisi.
"Jumamosi, Sakhpal alikutana na msichana huyo nje ya chuoni kwake huko Gorai na kumtaka amsindikize kwa matembezi kidogo. Wawili hao walipanda boti na kwenda kijiji cha Gorai," inspekta wa ngazi ya juu Deepak Bagawe alieleza.
Inspekta huyo alisema Sakhpal alijaribu kumshawishi mpenzi wake huyo wa zamani kurejesha mahusiano yao, lakini pale binti huyo alipokataa alidaiwa kutoa tindikali hiyo.
Kwa mujibu wa polisi, alidaiwa kumpanua msichana huyo mdomo na kujaribu kumimina tindikali hiyo ndani ya mdomo wake. Kiasi kidogo kilimwagikia usoni mwa binti huyo na kupata majeraha ya kuungua kwa asilimia 10-15.
Madaktari sasa wanajaribu kutathmini kiasi gani cha madhara ya ndani ya mwili aliyopata.
"Sakhpal anaonekana kuwa alipanga hayo kabla kutokana na kuwa amebeba kabisa tindikali hiyo," msaidizi wa kamishna wa polisi Mahesh Patil, alieleza.
Taarifa zinasema kwamba baada ya baba wa msichana huyo kulalamika kwa polisi kuhusu mvulana huyo, wawili hao waliripoti kwenye kituo cha polisi na 'kuandika kwamba hawatakutana tena na suala hilo limeshapatiwa ufumbuzi," alisema Deepak Bagawe, inspekta wa ngazi ya juu wa polisi wa Gorai.
Mmoja wa jamaa wa binti huyo alieleza: "Hapo awali tulifungua madai kuhusu kijana huyo. Alizoea kumtesa binti huyo na kumpiga hadharani. Alifikia hata kumtishia kumuua yeye na baba yake."
Hali ya binti huyo inaimarika lakini bado hawezi kutoa maelezo, kwa mujibu wa polisi walionukuliwa.
Ripoti zimedokeza kwamba baba wa msichana huyo anafanya kazi kwenye halmashauri ya mji huo wakati baba wa mvulana huyo ameajiriwa na kampuni binafsi

KASHFA...MBUNGE WA CCM MWENYE MIAKA 60 AFUNGA NDOA NA KIJANA MDOGO(KINDA)...

 Mbunge wa Viti Maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rosweeter Kasikila (60). 
MBUNGE wa Viti Maalumu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rosweeter Kasikila (60), amejikuta kwenye kashfa nzito ya kufunga ndoa na kijana, kinda wa miaka 26, Michael Christian.
Ndoa hiyo ambayo ilifungwa katika Kanisa la Tanzania Assembles of God (TAG), linaloongozwa na Mchungaji Getrude Rwakatare ambaye pia ni Mbunge wa Viti Maalumu kupitia CCM, imebaki kuwa gumzo na kuwaacha hoi baadhi ya mawaziri, wabunge wanaoifahamu pamoja na majirani wanaoishi na mbunge huyo.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya wanandoa hao na majirani wanaowazunguka, vililiambia gazeti hili kuwa ndoa hiyo ilifungwa Septemba Mosi mwaka 2011, na imebaki kuwa siri kabla ya wawili hao kukorogana.
Kabla ya wawili hao kuamua kufunga ndoa, mbunge huyo kutoka mkoani Rukwa, mwenye makazi yake Bagamoyo mkoani Pwani, alikuwa akimtumia Michael kwenye shughuli mbalimbali na muda wote alikuwa akiishi nyumbani kwa mbunge huyo.
Inaelezwa kuwa mbunge huyo ambaye ana familia ya watoto wawili ambao kiumri wanalingana na Michael, alianza uhusiano wa kimapenzi na kijana huyo kwa siri kubwa na baadaye alifanikiwa kumshawishi wafunge ndoa huku akimuahidi kumpa huduma mbalimbali anazotaka.
Kwa mujibu wa habari hizo, wawili hao waliamua kufunga ndoa katika Kanisa la TAG baada ya mbunge huyo kufanikiwa kumshawishi Mchungaji Rwakatare kwamba ndoa hiyo itakuwa siri, hasa kutokana na tofauti ya kiumri kati yao.
Hata hivyo ndoa hiyo kwa sasa imekumbwa na mgogoro mkubwa, huku mbunge huyo akidaiwa kuzuia kila kitu cha mumewe huyo, hasa vyeti vyake vya shule kama njia ya kumbana warudiane.

SOURCE: TANZANIA DAIMA

DOGO JANJA AFUKUZWA RASMI MTANASHATI ENTERTINMENT...TABIA MBAYA NDIO CHANZO

Msanii mdogo aliyewahi kutamba katika tasnia ya muziki wa bongo fleva Dogo Janja amefukuzwa rasmi Mtanashati Entertinment, Taarifa zilizofikia dawati letu la habari zinasema Dogo Janja amefukuzwa na Ostazi Juma Na Musoma baada ya kushindwana kitabia, Hapo awali Dogo Janja aliwahi kuwa mwanakundi la Tip Top Connection lililo chini ya uongozi wa Madee hata hivyo alifukuzwa na kurudi kwao Arusha ambapo Ustazi Juma Na Musoma alimfuata na na kumuweka kundini huku akimuhudumia katika kila jambo ambalo alitakiwa kupata kama
mtoto na mwanamuziki pia. Lakini Leo imefika tamati ya Ostazi Juma na kuamua kumuacha Dogo Janja aende zake.



Vile vile kutoka katika kundi hilo la Mtanashati Kuna nyimbo mpya ya msanii PNC inayokuja hivi karibuni, ni Bonge moja la track linakwenda kwa jina la HABARI YA MJINI, nyimbo hii itayoachiwa hvi karibuni itakuja pamoja na video kali. Jiandae kwa nyimbo kali kutoka kwa PNC


MAAJABU YA DUNIA..HII NDIO SHULE INAYOTOA MAFUNZO YA NGONO....

clip_image001[6]Hii ni shule ya kwanza inayotambulika rasmi Duniani kwa kutoa mafunzo ya ngono, ikifunza aina za mitindo ya kufanya ngono na namna ya kumuhudumia mwenza kwa mbinu mbalimbali.
Kwenye kila darasa katika kila shule mara zote hutokea kuwepo kwa mtoto ambaye huwa hafanya homework zake. Ndio maana ake, mpaka ilipokuja kutokea kufunguliwa kwa milango ya chuo hicho kilichopo Austria kwenye jiji la Vienna kinachojulikana kwa jina la Austrian International Séx School.

Shule hiyo hutoza £1,400 kwa temu moja, huku kikitoa mafunzo hayo kwa njia ya nadhalia na vitendo.
Wanafunzi wa shule hiyo huchanganywa na kuishi kwenye hostel moja ambapo hushauliwa wasaidiane kufanya ‘assignments’ zao.

Mkuu wa shule hiyo - Ylva-Maria Thompson - mtu ambaye huwezi mshangaa, ni nyota ya filamu za ngono na ni mtangazaji wa vipindi vya ngono kwenye TV.
Mwanamke huyo mwenye miaka 51 amesema: ‘Nia ni kuwafanya watu wawe wapenzi wazuri, kufahamu aina mbalimbali za mitindo ya kufanya ngono, namna ya kumshughulikia mwenza wako, kuzifahamu sehemu nyeti za mwili na kuwafundisha watu namna nzuri za ushiriki wa tendo la ngono.
Licha ya hivyo shule hiyo imekuwa ikipata vikwazo kadhaa, ambapo matangazo ya TV yanayoonyesha watu wakifanya ngono yamepigwa marufuku, huku wengi wakisema shule hiyo ipo kwa ajili ya kufanya biashara ya ngono.
Kuna yeyote anayependa kwenda kusoma shule hii japo kwa mwaka mmoja...?

JE, NI KWELI KUWA KILA MWANAMKE ANAJIUZA NA SIO WALE TU WANAOSIMAMA BUGURUNI??

Huu ni ukweli hata tukipinga hakuna mwanamke asiyejiuza tofauti kuna aina mbili tu za hii biashara.
1. Wale wanaojiuza kwa kutafuta wateja kusimama mabarabarani.2. Hawasimami barabarani wanaenda kwa special order, kufahamiana kwanza kama urafiki, kupitia mitandao, kukutana kwenye bar na magari n.k
Ukitaka kujua kuwa wote hawa wanajiuza, mlale mwanamke halafu usimpe noti uone zali litakavyokuwa! Fanya uchunguzi hapahapa jijini Dar, nakuhakikishia ni wanawake wachache sana labda 2%-10% ambao hawako kibiashara juu ya mapenzi.
1. Kuna demu mzuri sana anafanyakazi (ofisi kubwa) ya sirikali mshahara wake ni zaidi ya Tshs m2 kwa mwezi anabwana ake tena wameshibana lakini juzi tu akawa anataniwa na rafiki yangu mmoja mwenye nchi ndafuu sana kuwa nataka kukuoa, kama vipi uje home tuonje tunda bana, tena demu aliweka mafuta yake akaja na gari yake akavurugwa kisa uanjua nini hapa?? Pesa huyu anajiuza ila yeye ni kwa investiment huyu ni MUWEKEZAJI!!
2. Kuna demu anasoma chuo kikuu anatamba sana kwenye mitandao na kuweka picha ya bwana ake kila mara juzi kati mchizi wangu kamuanzishia chat kwa fb mpaka muda huu kashatoa uroda biashara ni ileile kila akitaka kutoa nauli, alipewa mara ya kwanza elfu 20 alikasirika sana, huyu ni mjasiriamali.
3. Nenda Bar yoyote Dar, hata mhudumu unayemuona anajiheshimu akikuletea soda au bia yako mnong'oneze mwambie nina lfu 50 tukalale wote, hakikisha una simu maana tayari mzigo umepata hii nayo ni biashara anauza sema tu ni parti time.
4. Usimuone mmama wa makamo mkubwa na mkurugenzi wa kampuni fulani mwambie ninajua kula mzigo lazima utampata tu wewe usiogope sura yake na heshima yake ongea tu, huyu naye anauza sema yeye ni doner.
5. Mademu karibia 80% Dar wanamabwana zaidi ya 5 kila mmoja amepengwa kisawasawa, kweli anao watano aende buguruni kufanya nini? 

Hata mkikataa mnajiuza tena mnajiuza vibaya sana dunia imeisha tu

MUUZA CHIPS AMTEKA MTOTO TANDALE DAR...ATOKOME BILA KUJUA ANAENDA KUMFANYIA NINI MTOTO HUYO

MTOTO wa kike mwenye umri wa miaka mitatu, Maryment Ibrahim ambaye anaishi Tandale jijini Dar es Salaam, hivi karibuni alipatwa na masahibu makubwa baada ya kutekwa nyara na kutoroshwa hadi Gairo mkoani Morogoro huku mtekaji akidaiwa kutaka apewe shilingi milioni 6 ili amuachie.
Mama mzazi wa mtoto aliyetekwa akiwa na mwanaye.
Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Oktoba 16 mwaka huu baada ya kijana mmoja, anayefanya biashara ya kuuza chipsi anayejulikana kwa jina la Issa Ramadhani, kudaiwa kumchukua mtoto huyo aliyekuwa akicheza nyumbani kwao na kutoweka naye kabla ya wazazi wake kubaini na kwenda kutoa taarifa kituo cha Polisi Kijitonyama ‘Mabatini’.
Awali, ilidaiwa Ramadhan alikuwa na tabia ya kuwachukua watoto wadogo wa mtaani hapo na kuondoka nao na kuwarudisha baadaye, kitu kilichowafanya wazazi wa mtoto huyo kutokuwa na wasiwasi.

Mtuhumiwa wa utekaji.
Wakizungumza na mwandishi wetu, wazazi wa mtoto huyo walisema waliamua kutoa taarifa polisi na kufunguliwa jalada nambari KJM/RB/8994/13 baada ya kupashwa kuwa mtekaji ambaye alishaacha kazi yake ya kukaanga chipsi, aliondoka muda mrefu na binti yao na hakukuwa na dalili za kurejea.
Baada ya kuhangaika kwa muda mrefu, wazazi hao pamoja na majirani walifanya uchunguzi wa chinichini na kufanikiwa kupata namba ya simu ya mtekaji huyo, lakini walifanikiwa kubadilishana naye ujumbe mfupi wa simu kwani hakuwa akipokea simu yake ya kiganjani.
Baba mzazi wa mtoto aliyetekwa akiwa na mwanaye.
Inadaiwa kuwa katika mawasiliano hayo, mtekaji alikataa katakata ombi la kumtaka amrudishe mtoto wao na kutaka apewe kiasi cha shilingi milioni 6 ili kutekeleza jambo hilo ingawa baadaye ilibainika jamaa huyo alikuwa Gairo mkoani Morogoro.
Wazazi hao walisema kuwa Oktoba 19 mwaka huu mmoja wa majirani walioguswa na tukio hilo aliyejitambulisha kwa jina la Justin Henry alijitolea kusafiri mpaka Gairo kumsaka mtoto na mtekaji wake jambo ambalo lilifanikiwa kwa kumpata mtoto akiwa mzima wa afya japokuwa mtekaji alishtukia na kukimbia.

HIVI NDIVYO MTANGAZAJI "JULIUS NYAISANGA" ALIVYOTESEKA....APIGANIA UHAI WAKE KWA SIKU 1460

NYOTA katika utangazaji Bongo, Julius Nyaisangah aliyefariki dunia Oktoba 20, mwaka huu katika Hospitali ya Mazimbu mjini hapa,  amepitia kipindi cha mateso cha takribani siku 1460 katika kupigania uhai wake.

Akizungumza , Jumatatu nyumbani kwake, Kihonda kulipokuwa na shughuli ya kumuaga marehemu Nyaisangah, mke wa marehemu, Bi. Leah Nyaisangah alisema mumewe alianza kusumbuliwa na ugonjwa wa Kisukari tangu mwaka 2009.
“Kama alikuwa nayo kabla hatujui lakini tuligundua kuwa mume wangu mpenzi ana sukari mwaka 2009 na baadaye ikagundulika pia alikuwa na shinikizo la damu, tangu hapo amekuwa akiteseka sana,” alieleza mama huyo akijitahidi kuzuia machozi.
 
Marehemu Nyaisangah enzi za uhai wake.
Alisema, licha ya kuugua mumewe alikuwa hodari wa kufanya kazi na kuendelea na majukumu yake muda wote katika Kampuni ya Abood Media aliyokuwa akifanya kazi mpaka mauti yalipomkuta.
“Kwakweli alijitahidi sana, alikuwa baba bora kwa familia yetu lakini Mungu amempenda zaidi. Namuombea makazi mema,” alisema.

MIEZI MITATU YA MATESO
Bi. Leah alisema, mumewe alikuwa akipatiwa matibabu katika hospitali mbalimbali mjini hapa na kuendelea na dawa lakini miezi mitatu iliyopita hali ilikuwa mbaya zaidi na alipumzika kwenda kazini kwa kipindi chote cha miezi mitatu.

“Lakini alipata nafuu na kurudi kazini, hadi wiki iliyopita alikuwa kazini kama kawaida ila sasa sukari ikapanda tena ghafla, halafu na presha nayo ikawa juu huku akiwa na malaria, ndipo akafariki,” alisema kwa uchungu.

RATIBA YABADILIKA
Awali, ratiba ilikuwa aangwe mjini hapa jana Jumanne kisha wasafari kwenda Tarime kwa  maziko yaliyotarajiwa kufanyika leo Jumatano lakini ilibadilika baada ya serikali kuomba mwili wake upelekwe Dar kwa ajili ya kuagwa na viongozi wa serikali pamoja na jamaa zake wa Dar.

Ujumbe kutoka Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo ulioagizwa na Naibu Waziri, Amos Makalla ulifika nyumbani kwa marehemu na kueleza nia ya wizara ambapo ulikubaliwa baada ya kushauriana na bosi wa Nyaisangah, Aziz Abood, ambaye pia ni Mbunge wa Morogoro Mjini.

MAMIA WAMUAGA MORO
Baada ya makubaliano hayo ambayo yalipata baraka kutoka kwa kamati ya mazishi, ililazimika kubadilisha ratiba haraka ambapo mwili ulichukuliwa Hospitali ya Mkoa Morogoro kwa ajili ya kuagwa ili usafirishwe kwenda Dar.

Wakazi wa Morogoro na vitongoji vyake walijitokeza kwa wingi juzi Jumatatu nyumbani kwa marehemu Kihonda na kutoa heshima zao za mwisho kabla ya safari ya kwenda Dar ambako mwili ulifikishiwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

DAR VILIO TUPU
Jijini Dar es Salaam, jana Jumanne, umati wa watu ulifurika kumuaga marehemu Nyaisangah, kabla ya kusafirishwa kwa ndege kwenda Tarime kwa maziko yaliyotarajiwa kufanyika leo.

Nyaisanga ameacha mjane, Leah na watoto watatu ambao ni Samuel, Noela na Beatrice.

AIBU...!! MUME NA MKE WA MTU WANASWA LIVE GESTI WAKINGONOKA BUGURUNI-SOKONI...

Live: Mume wa mtu, Emmanuel Benedict na mke wa mtu aitwaye Rehema baada ya kunaswa gesti saa 7 usiku.
Wawili hao walinaswa hivi karibuni kwenye gesti ambayo pia ina baa iitwayo Blue Roze maeneo ya Buguruni-Sokoni jijini Dar wakijiachia kwa raha zao.
Habari zilizopenyezwa katika timu yetu ni kwamba, baa hiyo hutumia vibaya leseni yake ya biashara kwa kugeuza gesti hiyo danguro ambapo machangu hufanya biashara ya kuuza miili yao katika eneo hilo.

Ilielezwa kuwa baa hiyo huwahifadhi machangudoa ndani yake huku biashara ya ngono ikifanyika mchana kweupe na usiku kucha bila kushtukiwa.
KAZI YAANZA
Ikiwa imebeba kauli ya Kamishina wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, CP Suleiman Kova kuhusiana na kukomesha biashara ya madanguro jijini, vijana wa OFM walitinga ndani ya baa hiyo kama wateja na kukamilisha uchunguzi wao ambao uliwapa jibu moja tu – biashara ya ngono inafanyika nje nje!
Wakati huohuo, kijana mwingine wa OFM aliingia upande wa gesti iliyopo ndani ya baa hiyo ili kupeleleza bei zake huku mhudumu akiahidi kupunguza bei kwa kuwa alikuwa na changudoa kutoka ndani ya baa hiyo tofauti na wengine waliokuwa wanatoka nje ya eneo hilo.
TAARIFA POLISI
Baada ya kujiridhisha kuwepo kwa hali hiyo, OFM ilitoa taarifa kwa Kamanda wa Polisi wa Wilaya ya Ilala, Lucy Kakulu ambaye haraka alimtaarifu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala, Marietha Minangi ambaye muda mfupi baadaye aliwasili kituoni hapo na kutoa baraka kwa OFM na kushiriki kuwachagua askari shupavu wa kufanya oparesheni hiyo.
Ilipotimia usiku wa manane, ndipo zoezi zima lilianza kwa mmoja wa mapaparazi wetu kuingia ndani ya baa hiyo na kupitiliza moja kwa moja hadi ndani ya gesti.
Akiwa ndani, paparazi huyo alifanikiwa kupatana na mmoja na kuingia naye chumbani huku akitoa ishara kuwa kila kitu kilikuwa wazi ni kiasi cha zoezi kufanyika tu.
KAZI IKAANZA
Kufumba na kufumbua askari shupavu wa Kituo cha Polisi  Buguruni, Dar sambamba na timu ya OFM waliingia mzigoni ambapo waliwanasa machangudoa na meneja wao aliyekuwa akizagaa ndani ya gesti hiyo.
Katika pekuapekua hiyo ndipo mume huyo wa mtu akanaswa laivu chumbani na mke wa mtu huku wote wakiomba msamaha kwa kuwa wana familia zao, hoja ambayo haikuwa na nguvu.

KILA MTU ANA NDOA YAKE
Katika kurusharusha miguu, mwanaume huyo alisema anaomba sana ishu hiyo iishie hapo, isifike polisi wala kwenye vyombo vya habari kwani ana ndoa na familia hivyo itakuwa ni aibu kubwa.
“Chondechonde mimi nina ndoa na familia jamani. Sijui nitaweka wapi sura kwa aibu. Naombeni tuyamalize kiutu uzima,” alisikika mwanaume huyo akijitetea kwa polisi, utetezi ambao haukumsaidia.
Katika mahojiano huku kondom zilizotumika zikiwa zimezagaa kila kona, kwa upande wa mwanamke alikiri kuwa alifanya tendo hilo bila kinga.
“Hatujazitumia sisi hizi, tumezikuta humuhumu chumbani. Lakini nawaombeni sana, msinipeleke polisi nina ndoa yangu. Naombeni mnisamehe kwa sababu mume wangu atanirarua. Ninyi wenyewe mnajua ndoa ilivyo ngumu, tafadhali naomba mnisitiri,” alisikika mwanamke huyo.
SAFARI YA POLISI
Pamoja na kuomba sana, polisi hao waliokuwa makini na kazi yao wakionekana kumuunga mkono vilivyo Kamanda Kova, waliwatilia ngumu na kuamua kuondoka nao wakiwa na pingu mikononi mwao.
Mbali na hao, oparesheni hiyo pia ilimtia nguvuni meneja wa eneo hilo, Emmanuel Mpinge, ambao wote kwa pamoja walifikishwa kituoni na kufunguliwa kesi yenye namba  BUG/RB/13114/2013 - KUFANYA VITENDO VYA UMALAYA 19/10/2013.

MSICHANA WA MIAKA 10 WA KIKATILI NA MWILI WAKE KUTUPWA CHOONI


MKAZI wa Kijiji cha Msanzi wilayani Kalambo katika Mkoa wa Rukwa , Festus Sungura (37) anadaiwa kumuua kikatili msichana Janeth Mwanandenje (10) na kisha kutumbukiza mwili wake ndani ya shimo la choo.

Inadaiwa choo hicho kilikuwa kikitumiwa na mkewe waliyetengana naye na lengo lilikuwa aweze kukamatwa na kufungwa kwa kosa la mauaji. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Jacob Mwaruanda alithibitisha kutokea kwa tukio hilo.
 
Alibainisha kuwa lilitokea Oktoba 18 mwaka huu saa 11 katika Kijiji cha Katuka Kata na Tarafa ya Matai wilayani Kalambo.
 
Mwaruanda alidai Oktoba 13 mwaka huu saa mbili usiku Janeth (marehemu) alikwenda kwenye ukumbi uliokuwa ukionesha mikanda ya video katika Kijiji cha Msanzi na hakurudi tena nyumbani kwao hadi mwili wake ulipogunduliwa ndani ya shimo la choo, kijiji jirani cha Katuka .
Inadaiwa siku iliyofuata, baba mzazi wa marehemu huyo aitwaye Mussa Mwanandeje , alitoa taarifa Kituo cha Polisi cha Matai ya kupotea kwa binti yake huyo.
 
Kwa mujibu wa Mwaruanda, Oktoba 18 mwaka huu jirani wa wazazi wa marehemu huyo katika Kijiji cha Msanzi, aitwaye Festus Sungura (37), alikwenda Kijiji cha Katuka, ambacho ni jirani na kijiji cha Msanzi.
 
Alikwenda kumfuata mkewe Rosemary Arusha, ambaye alirudi kwao kijijini hapo baada ya kugombana na mumewe huyo miezi kadhaa iliyopita.
 
Baada ya Sungura kufika Katuka, alikutana na binti yake aitwaye Digna Sungura (15), ambapo alimhoji iwapo mama yake mzazi ( mke wa Sungura) akifungwa, kwa kuwa anamchukia yeye baba yake, ataenda kuishi kwa nani? Binti yake huyo, alimjibu kuwa ataishi na bibi yake kijijini hapo Katuka.
 
Ndipo Sungura alipomwagiza binti yake huyo, akamwambie mama yake atoe miti mitatu, iliyowekwa juu ya shimo la choo wanachotumia, waone alichofakifanya yeye.
 
Mama ya binti huyo, alitoa taarifa kwa viongozi wa kijiji hicho cha Katuka, ambapo kwa kushirikiana na wakazi wengine, walitoa miti chooni hapo na kuuona mwili wa marehemu uliotumbukizwa humo.
 
Kwa mujibu wa Kamanda huyo, mtuhumiwa huyo ameshakamatwa na anatarajiwa kufikishwa mahakamani upelelezi wa shauri lake utakapokamilika.

KANISA LAVAMIWA JIJINI MWANZA..MUHUMINI MMOJA AUWAWA NA WENGINE KUJERUHIWA,CHEKI PICHA

 
Wananchi wakiwa wakitafakari nje ya jengo la Kanisa la Gilgal Christian Centre lililopo Pasiansi Ilemela jijini Mwanza.
 ----------
Mtu mmoja ameuawa na wengine watatu kujeruhiwa kufuatia shambulizi lililofanywa na kundi la watu wasiofahamika usiku wa kuamkia jana  katika kanisa la Gilgal Christian Worship Centre lililopo eneo la Pasiansi wilaya ya Ilemela jijini Mwanza.
Kamanda wa polisi mkoa wa  Mwanza , Ernest Mangu amethibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo mpaka sasa hakuna taarifa za kuibiwa kwa kitu chochote ndani ya kanisa, hali ambayo inalifanya tukio hilo kuwa na maswali mengi likihofiwa kufananishwa na yale ya uchomaji moto Makanisa.
Waumini wakitafakari tukio hilo la uvamizi lililosababisha taharuki  kwa wakazi wa jiji la Mwanza.
 
 
Ndugu na majirani pamoja na waumini waliomfahamu marehemu Elia Lunyamila aliyeuawa kwa kukatwa mapanga na watu wasiojulikana wakiwa wamekusanyika nyumbani kwa marehemu kuomboleza
 Askofu wa kanisa la Gilgal Christian Centre Eliabu Sentozi.
 

Tukio hilo lililotokea majira ya saa saba usiku linamtaja Elia Lunyamila (35) ambaye ni mlinzi  na ni  mwenyekiti wa vijana wa kanisa kuuawa akiwa amejumuika kwenye ibada na waumini wengine Alex Msakuzi na Tumsifu Pungu ambao hali zao zinatajwa kuwa taabani wakipatiwa matibabu Hospitali ya Rufaa Bugando Mwanza baada ya kujeruhiwa vibaya kwa kukatwakatwa mapanga sehemu mbalimbali za miili  yao. 
 
Askofu wa kanisa hilo Eliabu Sentoz amelaani tukio hilo akilitaja kuwa ni la kinyama kwani limefanyika sehemu ya ibada akiwataka wananchi kuungana pamoja kulisaidia jeshi la polisi katika kutoa taarifa kuwabaini wahusika wa shambulio  hilo na akaiomba serikali kuongeza nguvu kukabiriana na wahalifu hao.

KWELI BONGO FLEVA INALIPA TENA SANA, HEBU CHEKI PICHA ZA GARI MPYA ALIYONUNUA OMMY DIMPOZ


107
108
109
110
111
112
113
114
115
116
117
118
106
105
104
103
2
1


 

Copyright © 2009. MCHAMBUZI - Haki zote zimehifadhiwa